Our Project



Usafi  wa hedhi shuleni.


     
   -Historia ya Mradi  
        
        -Mnamo mwaka 2009-10 shirika la maendeleo la Uholanzi – SNV likishirikiana na wadau wengine wa maendeleo wakiwemo Water Aid na UNICEF waliwezesha wizara nne zikiwemo wizara ya elimu,afya, maji  na serikali za mitaa katika kuendeleza na kuongoza  miundombinu ya maji, mazingira na afya kwa kutumia miongozo ya Tanzania kwa njia shirikishi. SNV imekua ikitekeleza  miradi ya afya na maji shuleni kwa takribani wilaya 9 hapa Tanzania kwa kufuata muongozo wa SWASH



Shirika  la  SNV  kwa  kushirikiana  na    Halmashauri    ya  (W)  Magu,Sengerema,  Karatu,  Siha,  Mufindi,  Njombe,  Chato  na  Babati,lilifanya utafiti    katika  masuala  yanayohusiana na kupevuka  kwawatoto  wa kike   mashule ni.  Tafiti hiyo  ilionesha   kuwa wasichanawaliopevuka  na  wanaotazamia  kupevuka    hawana  taarifa    sahihiza  kutosha    juu  ya  upevukaji  na  wanatumia    njia  duni  zakujihifadhi  wakiwa  katika  hedhi.  Kipato  duni  kimechangiakuwepo  kwa    hali  ya  matumizi  mabaya    ya  bidhaa  za  kujihifadhikwa  watoto wa kike  wakati  wa  hedhi ambazo zimepelekea  kuwepokwa changamoto katika kujihifadhi vizuri, kwa usalama  na usafi.Utafiti  ulibaini  zaidi  ya  60%  ya  wasichana  walio  katika  hedhihawatumii  pedi  sahihi  na  salama  wanapokuwa  katika  siku  zao.Hali  hii  imesababisha  wasichana  wengi  kudhalilika  hasa  paleinapojitokeza pasipo na maandalizi ya kukabiliana nayo.

Hali  hii  imesababisha  utoro  mashuleni  hasa  kwa  watoto  wa  kikekwa  muda  wa  siku  3  hadi  7  kila  mwezi.  Mazingira  hayayamepelekea baadhi ya watoto wa kike wanaosoma katika shule zamsingi ku kosa vipindi vya masomo  kwa wastani wa vipindi kati ya240  hadi  560;  na  kwa  wanaosoma  katika  shule  za  sekondarihukosa  vipindi  kwa  wastani  wa  kati  ya  180  mpaka  430  kwa  kilamwaka wa masomo.

Zaidi  ya  70%  ya  wanafunzi  wa  kike  waliofikia  umri  wa  kupatahedhi  wamethibitisha  kutokufanya  vizuri  katika  masomo  yao  nawengine kushindwa kumaliza masomo yao.
 Hivyo  vijana  wa  kike  wanahitaji  elimu  ya  afya  na  usafi  wa  hedhikwa  kiasi  kikubwa.  Utafiti  uliofanywa  na  shirika  la  SNV    katika wilaya hizo kwa kushirikiana na Halmashauri, zinaonesha kuwepoShirika  la  SNV  kwa  kushirikiana  na    Halmashauri    ya  (W)  Magu,Sengerema,  Karatu,  Siha,  Mufindi,  Njombe,  Chato  na  Babati,lilifanya utafiti    katika  masuala  yanayohusiana na kupevuka  kwawatoto  wa kike   mashule ni.  Tafiti hiyo  ilionesha   kuwa wasichanawaliopevuka  na  wanaotazamia  kupevuka    hawana  taarifa    sahihi za  kutosha    juu  ya  upevukaji  na  wanatumia    njia  duni  za kujihifadhi  wakiwa  katika  hedhi.  Kipato  duni  kimechangia kuwepo  kwa    hali  ya  matumizi  mabaya    ya  bidhaa  za  kujihifadhi kwa  watoto wa kike  wakati  wa  hedhi ambazo zimepelekea  kuwepo kwa changamoto katika kujihifadhi vizuri, kwa usalama  na usafi. Utafiti  ulibaini  zaidi  ya  60%  ya  wasichana  walio  katika  hedhi hawatumii  pedi  sahihi  na  salama  wanapokuwa  katika  siku  zao.
Hali  hii  imesababisha  wasichana  wengi  kudhalilika  hasa  pale inapojitokeza pasipo na maandalizi ya kukabiliana nayo.Hali  hii  imesababisha  utoro  mashuleni  hasa  kwa  watoto  wa  kike kwa  muda  wa  siku  3  hadi  7  kila  mwezi.  Mazingira  haya yamepelekea baadhi ya watoto wa kike wanaosoma katika shule za msingi ku kosa vipindi vya masomo  kwa wastani wa vipindi kati ya 240  hadi  560;  na  kwa  wanaosoma  katika  shule  za  sekondarin hukosa  vipindi  kwa  wastani  wa  kati  ya  180  mpaka  430  kwa  kila mwaka wa masomo.

Zaidi  ya  70%  ya  wanafunzi  wa  kike  waliofikia  umri  wa  kupata hedhi  wamethibitisha  kutokufanya  vizuri  katika  masomo  yao  na wengine kushindwa kumaliza masomo yao.Hivyo  vijana  wa  kike  wanahitaji  elimu  ya  afya  na  usafi  wa  hedhi kwa  kiasi  kikubwa.  Utafiti  uliofanywa  na  shirika  la  SNV    katika wilaya hizo kwa kushirikiana na Halmashauri, zinaonesha kuwepo na uhitaji mkubwa wa kujenga uwezo wa kujitambua na kujimudu kiafya,  wanapoingia  katika  hedhi,  hasa  katika  shule  za  msingi.Hivyo, uelewa mzuri wa afya na usafi wa hedhi utasaidia vijana wa kiume na  wa kike, kuwa  na  maamuzi  na  mtazamo chanya  katikamasuala yote yanayohusiana na afya na usafi wa hedhi.



Katika kutekeleza mradi, Tanzania Cares (TZC) wamekabidhiwa dhamana ya utekelezaji  na usimamizi wa mradi katika wilaya(Magu). 

Lengo la Mradi

  • ·         Kuongeza matumizi ya pedi za kisasa kwa wanafunzi wa kike kwa shule za vijijini na pembezoni mwaa miji



Malengo Mahususi:-
 
  •  Kuongeza namba ya wanafunzi wa kike wanaopata na kutumia pedi za kisasa kirahisi
  •  Kuongeza uelewa wa masuala juu ya elemu ya hedhi na usafi wa mwili kwa wanafunzi wote (wa kike na wale wa kiume) 
  •   Kuongeza  faida ya elimu kwa wanafunzi wasichana na wanafunzi wengine  (hususani katika mahudhurio,kumaliza na kiwango cha ufaulu)
  •   Kuandaa na kutengeneza vipindi vitakavosaidia kuinua na kuboresha masuala ya elimu juu ya masuala  ya hedhi na usafi (katika kuratibu, kulinganisha na kuangalia ubora wa vifaa vinavyotupatikana.  

Utekelezaji wa  Mradi 



  1.          Kutambulisha mradi kwa kamati ya maji na usafi ya wilaya (CWST) kwenye  halmashauri pamoja na kuchagua shule zitakaanzo anza kujengewa uwezo
     2. Kuwajengea uwezo Waalimu wa afya na kamati za shule juu ya ukubwa wa tatizo pamoja na        kufikia maazimio juu ya majukumu yao katika kufanikisha mradi huu katika:-   
Hii ilikuwa ni semina ya walimu wa afya shuleni na wajumbe wa bodi na kamati za shule.
       

- Kumwelekeza mzazi kutengeneza mazingira rafiki na binti/kijana
-  Kumwandaa binti katika hali ya kujiamini na kujitunza pindi aingiapo katika hedhi katika mazingira yoyote (shuleni/nyumbani)
-  Kuwashauri wazazi kuwa mifano halisi juu ya hali ya usafi wa hedhi
- Kutenga bajeti katika masuala ya hedhi kwa watoto wao kila mwezi
-  Kutoa mapendekezo kwa kuwashirikisha wazazi na wadau wa maendeleo juu ya namna ya upatikanaji wa pedi shuleni
-  Kuvunja ukimya katika suala zima la hedhi kwa watoto wao.
3. Kuwajengea uwezo  waalimu wakuu na waratibu wa elimu kata katika shule za msingi 
              na  sekondari.                                                                                                                              
       4. Kuwajengea uwezo madiwani na kuwashirikisha katika mpango mzima wa uchangiaji gharama        
             katika upatikanaji na garama nafuu wa pedi shuleni)                                                                                                                                                     
                                 



Washiriki wa utekelezaji mradi


Shirika la maendeleo la Uholanzi - SNV na  Tanzania Cares  (TZC)


            Eneo la mradi

Wilaya ya Magu, kata za: Nyigogo, Kitongosima, Kongoro, Nkunguru, Nyanguge, kahamgara, Magu mjini, lutale na Lubugu ambapo jumla ya shule 21;  za msingi zikiwa 11 na za sekondari 10 zimehusishwa.



   Maendeleo ya mradi


Kazi ambazo zimekwisha kufanyika hadi sasa ni:
  •   Kuutambulisha mradi katika halmashauri husika (Magu)
  • Kutembelea shule 21 katika kata 9 kwa ajili ya utambulisho wa mradi
  • Makundi ambayo yameshajengewa uwezo katika kata za mradi ni pamoja na:  
                             -Waalimu wa afya na walimu wakuu wa shule
                                                         -Kamati  na bodi za shule
                             -Waratibu elimu kata               
                                                        -Madiwani 
  •            Kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wanaohusika moja kwa moja kwenye huu mradi katika ngazi tofauti tofauti (waalimu wakuu na walimu wa afya na malezi katika shule zilizoteuliwa, waratibu elimu kata, wajumbe wa bodi na kamati mbalimbali za shule katika wilaya husika.    


 




Mafanikio yaliyopatikana katika kazi ambazo zimekwisha kufanyika ni pamoja na:-


          Uhamasishaji umefanyika katika ngazi mbalimbali na kupokelewa vyema kuanzia halmashauri, kata na ngazi ya shule jambo linaloonesha kuwepo mwanga na  mwanzo mzuri katika kufanikisha mradi.







 

 

 

0 comments:

Post a Comment